Machapisho

MPENZI BORA.

Picha
    Picha: Hisani ya Dreamtimes.com Sikia mpenzi sikia, ewe wangu wa ubani Wewe ndiwe malkia,  nikuenziye moyoni Habibi nakusifia,  wangu namba wani Nakupenda wangu muhibu,  mwingine sitamani. Usojua kukasirika,  vipodozi wala kupara Mwenziyo nachacharika,  unipigapo mikwara Umeniteka hakika,  nakughania mikarara Nakupenda wangu muhibu,  mwingine sitamani. Mama huna maringo,  wala pesa kutakia Kifua chako mviringo,  lazizi wanivutia Halafu yako shingo,  tisti imesimamia Nakupenda wangu muhibu,  mwingine sitamani. Siwatamani kabisa, warembo wa humu mjini Naogopa watanitosa, huwapati mapenzini Punde pesa nikikosa, watatoroka nyumbani Nakupenda wangu muhibu,  mwingine sitamani. Kipi sikipati kwako, mwendani wangu wa dhati Mtima mehamia kwako, nikande kama chapati Niamini mimi wako,  moyo unapuma ati Nakupenda wangu muhibu,  mwingine sitamani. Kwanza huo wako mwanya, mwenzio najiishia Unazo fikira chanya, wanipa...

NIKUSAMEHE UKAE WAPI?

Picha
Picha: 123rf. Nakumbuka siku zile, makuzi 'kinifanyia Kijijini kwenu kule, kwenu ulikokulia Sitokulaumu vile, mandhari ulozukia Nikusamehe ukae wapi, na moyo wangu uliuchana? Uliniona mdogo, kamwe sikutoshelezi Ikakujaa mikogo, kunionyesha ushenzi Na kumshika pembe mbogo, kwenye sehemu telezi Nikusamehe ukae wapi, na moyo wangu uliuchana? Ulidhani kuniacha, utaua nyota yangu Kama ndimu umechacha, watafuta namba yangu Kucha zako ulificha, ukadunga moyo wangu Nikusamehe ukae wapi, na moyo wangu uliuchana? Uliacha ngalawa, kisa muogeleaji Kila siku ulilewa, ukavujisha mfereji Ulijaa na kukupwa, kama ya bahari maji Nikusamehe ukae wapi, na moyo wangu uliuchana? Hivi sasa sikutaki, katafute kifu yako Atayekupa malaki, ufurahi nafsi yako Peke yangu nitabaki, si lazima penzi lako Nikusamehe ukae wapi, na moyo wangu uliuchana?